Monday, April 13, 2015

Costa kuwafanyia unoko Arsenal


 
In Summary
Chelsea haina haraka ya kumrudisha uwanjani Costa kwa hofu kuwa anaweza apate maumivu zaidi, lakini mwenyewe anataka kucheza mchezo huo dhidi ya Arsenal. Fowadi huyo hakumaliza mechi na Stoke City baada ya kuumia
HUU sasa unoko. Straika, Diego Costa amesema atajikaza na kuweka kando maumivu yake ya misuli ili kuhakikisha anacheza dhidi ya Arsenal katika mchezo ambao Chelsea inaamini ndiyo utakuwa mwisho wa mbio za ubingwa wa Ligi Kuu England msimu huu.
Chelsea haina haraka ya kumrudisha uwanjani Costa kwa hofu kuwa anaweza apate maumivu zaidi, lakini mwenyewe anataka kucheza mchezo huo dhidi ya Arsenal. Fowadi huyo hakumaliza mechi na Stoke City baada ya kuumia.
Kocha Jose Mourinho alimfuta fowadi huyo kwenye kikosi chake kwa wiki mbili kwa maana kwamba atakosa mechi dhidi ya Queens Park Rangers na Manchester United huku kocha huyo Mreno akiwaza pia uwezo wa kikosi chake kwenye safu ya ushambuliaji kucheza bila ya staa huyo licha ya sasa kuongoza ligi kwa tofauti ya pointi saba.
Arsenal kama itateleza kwenye mechi ya wikiendi hii dhidi ya Burnley itaipa nafasi Chelsea kimahesabu kujisogeza kwenye ubingwa kabla ya kwenda kumenyana nao Aprili 26, lakini kama tu watakuwa wamezishinda QPR na Man United.
Hata hivyo, hata kama Arsenal wataichapa Burnley kuna imani kubwa Stamford Bridge kwamba ushindi watakaopata Emirates utawasogeza kwa asilimia kubwa kwenye ubingwa kitu ambacho Costa anataka kuwamo kwenye mchezo huo.

No comments:

Post a Comment