Thursday, April 16, 2015

Mbunge wa Jimbo la Moshi mjini Philemoni Ndesamburo akimtambulisha Mstahiki Meya wa Manispaa ya Moshi Jafary

Mbunge wa Jimbo la Moshi mjini Philemoni Ndesamburo akimtambulisha Mstahiki Meya wa Manispaa ya Moshi Jafary kuwa mrithi wake wa kiti cha ubunge katika jimbo hili wakati wa uchaguzi mkuu utakaofanyika mwezi oktoba.

Ndesamburo akizungumza na wananchi wa Moshi mara baada ya kumtangaza mrithi wake katika jimbo la Moshi mjini.


Mwakilishi wa Kudumu wa Tanzania katika Umoja wa Mataifa, Balozi Tuvako Manongi akibadilishana mawazo na Bw. B. Lynn Pascoe ambaye ni kati ya wajumbe 14 wa Tume Huru iliyoundwa na Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa kufanya tathmini kuhusu hali ya sasa ya Operesheni za Ulinzi wa Amani pamoja na Misheni Maalum za Kisiasa. Tume hiyo huru iliyoteuliwa mwishoni mwa mwaka jana imekwisha anza kazi.
Jana ( Jumatano ) Baadhi ya wajumbe wa Tume hiyo akiwamo Bw. Pascoe walikutana katika majadiliano yasiyorasmi na Wawakilishi wa Kamati Maalum ya Nne ya Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa na kubadilishana mawazo kuhusu masuala ya jumla yahusuyo Misheni Maalum za Kisiasa. Mkutano huo uliandaliwa na Idara ya Siasa ya Umoja wa Mataifa.
Akichangia majadiliano hayo, Balozi Manongi, amesema kwamba Misheni Maalum za Kisiasa, pamoja na umuhimu wake na mchango wake katika mustakabali wa amani na usalama, lakini ni misheni ambazo zimekuwa zikilalamikiwa na nchi wanachama, hasa kutokana na ukweli kwamba uundwaji wake hauko wazi, si shirikishi wala jumuishi.
Kutokana na mazingira hayo, Balozi Manongi ameishuri Tume hiyo Huru kuliangalia kwa mapana suala la Misheni Maalum za Kisiasa ikiwa ni pamoja na muundo wa uundwaji wake na pia kuboresha uwazi, uwajibikaji na uwakilishi utakaozingatia uwakilishi jumuishi wa kila kanda.

No comments:

Post a Comment