Mtanzania aliyekamatwa Kenya akidaiwa kufanya ugaidi katika Chuo Kikuu cha Garissa uliosababisha vifo vya watu 148, Rashid Charles Mberesero (20) ni mwanafunzi wa kidato cha tano, lakini uongozi wa shule anayosoma umesema alitoweka shuleni hapo Desemba Novemba 2014.
Habari
zilizothibitishwa na wazazi wake ni kuwa mwanafunzi huyo anasoma katika
Shule ya Sekondari ya Bihawana, Dodoma, baada ya kufaulu katika Shule
ya Sekondari Gonja mkoani Kilimanjaro.
Mama mzazi wa
kijana huyo, Fatuma Ali alisema jana kuwa: “Baada ya kufaulu
alichaguliwa kujiunga na Sekondari ya Bihawana na likizo alirudi
nyumbani na baada ya likizo kuisha aliniaga anarudi shuleni.”
Taarifa
hizo zimekuja wakati Mberesero maarufu kwa jina la Rehani Dida,
akitarajiwa kufikishwa mahakamani leo jijini Nairobi baada ya watuhumiwa
wengine kufikishwa mahakamani juzi.
Mwendesha
mashtaka, Daniel Karuri alisema, “Rehani Dida” hakufikishwa kortini
kwani alikuwa na wapelelezi mjini Garissa kukusanya ushahidi zaidi,
baada ya kukiri kuwa ni mfuasi wa kundi la Al-Shabaab.
Mtanzania
huyo anadaiwa kukamatwa baada ya kujificha kwa saa nane akiwa
amejichanganya na maiti, lakini baadaye alipanda na kujificha darini
akiwa na mabomu.
Kauli ya wazazi
Jana,
mama huyo, aliwaambia waandishi wa habari kuwa haelewi ni nani aliyemshawishi
mwanaye kujiunga na kundi hilo na kwamba jambo hilo limemshtua.
“Hizi
taarifa tumezisikia na kuona kwenye TV na kwa kweli zimetushtua sana,
mimi nahisi huko shule ndiko alikokutana na watu wabaya,” alisema Fatuma
ambaye ni mkazi wa Gonja wilayani Same.
Baba mzazi wa
mtuhumiwa huyo, Charles Mberesero Temba, alikiri kuwa Rashid ni mtoto
wake ambaye alizaa na Fatuma mwaka 1994 na miaka yote alikuwa akiishi na
mama yake.
“Huyo mtoto sijawahi kuishi naye, muda wote
tangu 1994 alikuwa akilelewa na mama yake,” alisema Temba na kuongeza
kuwa hakuwahi kuishi na mzazi mwenzake huyo.
No comments:
Post a Comment