
Na Rahma Khamis /Takdiri Ali- Maelezo Zanzibar
Wizara ya
Afya Zanzibar imesema Kitengo cha Mifupa katika Hospitali ya Mnazi
Mmoja kinaendelea kufanya kazi zake za kutoa Matibabu Masaa 24
kama kawaida kwa kufuata utaratibu maalum uliowekwa Hospitalini hapo.
Hayo
yameelezwa na Naibu Waziri wa Afya Mahmoud Thabit Kombo huko katika
Ukumbi wa Baraza la Wawakilishi Chukwani wakati alipokuwa akijibu swali
la Mwakilishi wa Jimbo la Muyuni Jaku Hashim Ayoub aliyetaka kujua lini
Serikali itaweka daktari katika Hospitali hiyo kwa Masaa 24.
Amesema
Hospitali ya Mnazi Mmoja ni Hospitali Pekee ya Rufaa kwa Zanzibar ambayo
inafanya kazi ya kutoa huduma bora za afya na kwamba kwa sasa
ina Madaktari bingwa wa Mifupa Wawili wanaopatikana kwa muda wa Masaa 24
No comments:
Post a Comment