Mwili wa
aliyekuwa Mbunge wa Ukonga, Eugen Mwaiposa ukiwasili kwenye viwanja vya
Bunge mjini Dodoma kwa ajili ya kuagwa jana. (Picha na Mohamed Mambo)
WABUNGE
jana walikuwa na wakati mgumu kuzuia machozi kutiririka katika nyuso zao
wakati jeneza lililobeba mwili wa Mbunge wa Jimbo la Ukonga jijini Dar
es Salaam, Eugen Mwaiposa lilipokuwa likiingia katika viwanja vya Bunge
kwa ajili ya mazishi.
Wengi wao
wakiwa wamevalia vazi jeusi ikiwa ni alama ya maombolezo na wengine,
hasa wanawake kuvalia khanga, waliangua vilio wakati mwili huo ukiingia
viwanjani ukiongozwa na Mbunge wa Viti Maalumu, Esther Bulaya (CCM)
aliyekuwa amebeba msalaba.
Haukuwa
uso tu wa Bulaya ulioonesha kutatizwa, bali na mwili wake wote haukuwa
sawa sawa, ukionesha kubeba majonzi makubwa kwa msiba huo.
No comments:
Post a Comment