
KATIBU
Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Abdulrahman Kinana amehadharisha
Halmashauri ya Manispaa ya Bukoba dhidi ya mpango wake wa kujenga soko
la ghorofa kwa kuitaka ijifunze kilichoikumba Halmashauri ya Jiji la Dar
es Salaam baada ya kujenga soko la Machinga Complex .
Hadhari
hiyo aliitoa juzi katika mkutano wa hadhara katika eneo la Kashai, mjini
Bukoba, baada ya kupokea taarifa ya halmashauri hiyo juu ya mpango wake
wa ujenzi wa soko jipya la kisasa.
Kinana
ambaye alihimiza watendaji kuhakikisha utekelezaji wa mpango wa ujenzi
wa masoko unakuwa shirikishi kuepuka migogoro na hasara, alisema
wafanyabiashara wana uwezo wa kushauri ni muundo gani wa soko unawezesha
kupata wateja. Baada ya kupokea taarifa hiyo ya halmashauri ikitaja
mpango wake wa kujenga soko la ghorofa, Kinana alisema, "Mimi sijawahi
kuona soko lenye ghorofa .
Nimezunguka
nchi hii sana, Arusha, Tanga, Dar es Salaam nenda pale Kariakoo hakuna
ghorofa." "Kwa nini nasema hivi? Kuna soko limeanzishwa Dar es Salaam
linaitwa Machinga Complex, lina ghorofa mpaka juu sasa wameshindwa
kulipa kodi.
Kwa
sababu, nani yuko tayari kupanda ghorofa ya sita kwenda kununua
chumvi...kwa nini asinunue chumvi barabarani kwa hiyo jihadharini,"
alisema.
Aliwaambia
kwamba wanaweza kujenga ghorofa wakajikuta ghorofa ya juu haina mtu na
ya chini ndiyo yenye watu wengi wakati huo huo madeni yakawa yamewakaba
koo. "Halafu mnaanza kuwaambia wananchi tunapandisha kodi ili mlipe deni
. Wanaolipa wananchi, waliokopa wakubwa. Hapana.
Changamsheni
bongo ili wananchi wasiumie,” alishauri na kusisitiza ushirikishaji wa
wafanyabiashara katika utekelezaji mpango huo. “Msiamue mambo wenyewe
fuateni ushauri kutoka kwa wafanyabiashara watawaambia.
Nani
anaweza kwenda kununua khanga ghorofa ya nne wakati barabarani ipo? Nani
atakwenda kununua nyanya ghorofa ya pili wakati chini nyanya zipo?
Awali,
katika risala ya wafanyabiashara wa Soko Kuu la Bukoba kupitia umoja
wao, waliokuwa kwenye mvutano na halmashauri juu ya uamuzi wa kujenga
soko hilo jipya, walisema hawapingi maendeleo bali wanaomba
washirikishwe upatikanaji wa soko jipya kabla ya utekelezaji wa mpango
huo
No comments:
Post a Comment