Percy
Sledge nyakati zake Mwanamuziki chapa 'Soul' aliyetikisa ulimwengu kwa
miaka mingi kutokana na utunzi wake ''When a Man Loves a Woman'',Percy
Sledge ameaga dunia.
Raia huyo wa Marekani aliaga dunia akiwa na umri wa miaka 73 nyumbani kwake Baton Rouge, Louisiana.
Afisa wa muungano wa wasanii Steve Green, ameithibitishia BBC kifo cha muimbaji huyo nguli.
Wimbo
wake uliovuma kote duniani kwa miaka na mikaka '' When a Man Loves a
Woman'' uligonga orodha ya kumi bora mara mbili nchini Uingereza.
'' When a
Man Loves a Woman'' uligonga orodha ya kumi bora mara mbili nchini
Uingereza Sledge aliyewahi kuvuma katika runinga ya BBC Two mwaka wa
1994 kwa ushirikiano na Jools Holland alishikilia nafasi ya kwanza kwa
majuma mawili mfululizo alipozindua wimbo huo''When a Man Loves a
Woman'' mwaka wa 1966.
Muimbaji huyo pia alitesa sana nchini Uingereza wimbo wake huo ulipopanda hadi nafasi ya nne katika jedwali la kumi bora.
Na
haikuishia hapo Percy Sledge, alirejea kwa kishindo mwaka wa 1987
alipotoa nakala ya wimbo huo na mara utunzi wake ukabobea kwa mara
nyengine tena nchini Uingereza.
Wimbo huo ''When a Man Loves a Woman'' ulivuma na kuwa wapili kwa umaarufu nchini Uingereza.
Sledge
alisherehekea miaka 49 tangu alipotangazia ulimwengu wa Muziki wa Soul
kuwasili kwake na wimbo huo ''When a Man Loves a Woman''.
Sledge
aliwahi kuwa muuguzi kabla ya kufuata talanta yake na kuibukia kuwa
muimbaji hodari. Bwana huyo aliweka historia alipoandikwa katika daftari
la wanamuziki waliobobea yaani '' Rock and Roll Hall of Fame katika
mwaka wa 2005''.
Sledge alikuwa mwanachama wa muungano wa wanamuziki kutoka Alabama.(V.S)
No comments:
Post a Comment