Waziri wa mambo ya nje Bernad Membe
SIKU
chache baada ya kuwarudisha nchini Watanzania 25 kutoka Yemen, Serikali
imetangaza kuwarudisha nyumbani Watanzania wengine 64 waliokuwa huko,
ili kuwaepusha na machafuko yanayoendelea nchini humo.
Katika
taarifa iliyotolewa jana jijini Dar es Salaam na Wizara wa Mambo ya Nje
na Ushirikiano wa Kimataifa, serikali imefikia hatua hiyo ili kuwanusuru
raia wake na machafuko nchini humo.
Taarifa
hiyo ilisema Waziri wa wizara hiyo, Bernard Membe yuko nchino Oman kwa
ziara ya siku moja na alizungumza na Balozi wa Tanzania nchini humo, Ali
Ahmed Saleh, na kusema serikali ina jukumu la kuhakikisha usalama wa
raia wake.
"Nimeruhusu
matumizi ya fedha ya dharura ili kuhakikisha ndugu zetu walioko kwenye
hatari na machafuko huko Yemen wanarejeshwa salama nyumbani mara moja,"
alisema Membe.
Alisema
raia hao ambao wengi ni wanafunzi, watarejea nchini salama na hiyo ni
kufuatia kupewa kwao ruhusu ya kuingia nchini Oman.
Na
kuongeza, siku chache zilizopita, watanzania 25, walirudishwa nchini
kutoka Yemen chini ya utaratibu wa Ofisi za Ubalozi wa Tanzania mjini
Muscut,Oman, na sasa awamu hii watarudishwa raia 64.
Taarifa
hiyo pia ilisema, hivi sasa wanafunzi hao wamefika kwenye mji wa Sarfat
na Al-Mazyouna iliyopo mpakani mwa Oman na Yemen.
Katika
taarifa hiyo, Membe alisema Watanzania hao ambao wengi wao hadi sasa
wamefika miji ya Sarfat na Al-Mazyouna, walituma maombi ya dharura
kwenye Ofisi za Ubalozi kuelezea mazingira ya hatari yanayowakabili,
ambapo zoezi la kuhakiki, kuandikisha na kuwarudisha lilianza mara moja
No comments:
Post a Comment